Uamuzi wa ACT Wazalendo kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
Posted by data tz
on Tuesday, June 6, 2017
0
Uamuzi wa ACT Wazalendo kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

Tarehe 03 Juni 2017 Chama chetu kilipokea taarifa kuhusu uteuzi Mama Anna Elisha Mghwira, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Uteuzi wa Mwenyekiti wetu umefanywa akiwa nje ya nchi na baada ya kurejea amefanya mazungumzo na viongozi wenzake wa juu wa Chama kuhusu uteuzi wake huo.
Kufuatia uteuzi huu na kwa kuzingatia unyeti na majukumu ya Mkuu wa Mkoa, Kamati ya Uongozi ya chama itakutana kesho tarehe 07 Juni 2016 kutafakari pamoja na mambo mengine, namna ambavyo Mama Anna Mghwira atatekeleza wajibu wake wa uenyekiti wa chama na majukumu yake mapya.
Chama kinatoa wito Kwa wanachama wote kuendelea na utulivu wakati vikao vya Chama vinachukua hatua stahiki kuhusu jambo hili.
Ado Shaibu,
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma,
ACT Wazalendo.
Imetolewa leo tarehe 06 Juni 2017
Tagged as: HABARI TANZANIA
Ni mtandao wa Kuhamasisha,Kuwawezesha Wajasirimali wadogo na wakubwa waweze kupata soko la Bidhaa/Huduma zao kwa Njia ya mtandao wa internet. Tunawatengezea vitabu, mashapisho na kurasa za Facebook, Instagram, Twitter. Wasiliana nasi kwa Email datatz88@gmail.com Simu 0763491136/0714067875/0688496762
Asante na Karibu Sana.
Jiunge Nasi
Jiunge nasi Upokee makala za kuhamasiha moja kwa moja kwenye email yako
Share This Post
Related posts
0 comments: