Miliki Website / Blog / PhoneApp

 Image result for what is blog Image result for website

 

 Image result for phone appImage result for phone app

Website/Blog  ni nini? 

Website/Blog ni mtandao/tovuti/ukurasa ambao unatumia kuweka habari endelevu za mara kwa mara. Mtandao huu unalenga Zaidi kumilikiwa na mtu mmoja au kikundi kidogo cha watu.

Blog ni rahisi kutumia kuliko tovuti nyingine za kawaida huhitaji mtu wa IT kwa ajili ya kukuendeshea unaweza kutumia mwenyewe na kuendesha mwenyewe.


Blog haina gharama kubwa za kuendesha kama wewe ndio unaanza unashauriwa kumiliki blog aina ya kawaida kabisa ambayo hulipii chochote Zaidi ya gharama za kutengenezewa nayo itakua kama hivi www.datatz1.blogspot.com  hiyo ni blog ambayo utatumia bure hadi utakapoamua kubadilisha na kulipia domain ambapo itakua hivi www.datatz1.com  ni wewe mwenyewe kuchagua aina unayotaka ila kwa wale ambao bado kabisa ndio wanaanza kutumia mtandao huu nawashauri kuchukua ambayo haina malipo ya mwezi ili kupata uzoefu kwanza.




Blog ni nzuri kwa kutunza kumbukumbu zako haijalishi unaandika kitu gani kwa kupitia blog utaweza kutunza kumbukumbu zako muda mrefu sana bila kupoteza na ni sehemu ambayo hakuna wa kukuingilia wewe ndio mmiliki. Ni sawa na ofisi yako ni sehemu ambayo wewe unaamua uweke nini na ukitunze vipi.

Mtu gani anatakiwa amiliki blog? Naweza kusema ni kila mtu ambaye anafanya vitu vinavyomkutanisha na watu. Haijalishi ni biashara, kazi yako, kipaji chako, au chochote kile kumiliki blog ni muhimu kwasababu uliwengu wa sasa unahamia kwenye mtandao kama huna mtandao utaachwa nyuma sana.

Blog haihitaji uwe na uelewa mkubwa sana wa IT. Watu wengi wanaogopa kwamba hawataweza kuendesha blog kwakua hawajui kutumia computer ukweli ni kwamba mambo ni marahisi sana unaweza kuendesha blog kwa kutumia smartphone yako, tablet na computer ni ufahamu kidogo sana unahitajika juu ya uendeshaji.



Mitandao ya kijamii.

Kitu cha pili ambacho ni muhimu kua nacho ni kurasa kwenye mitandao ya kijamii kurasa hizi zinakuwezesha wewe kuwaelekeza watembeleaji wako kwenye blog yako. Kuna aina mbalimbali ya mitandao ya kijamii kama Facebook. Twitter Instagram, Whatsapp na Telegram. Watu wengi  wamekua na matumizi mabaya na hii mitandao. Naomba wewe usiwe mmoja wao itumie mitandao hii kwa namna bora ya kusaidia watu na wewe mwenyewe uweze kupata manufaa. Tumia vyema wale watu unaokutana nao ili uweze kunufaika na wao wanufaike pia. 

Kama ni biashara utahitaji uwe na ukurasa kwenye Facebook ukurasa ambao utasimama kwa jina la biashara yako. Utajieleza ni kitu gani unafanya na watu wakaotembelea ukurasa huo watapata mawasiliano yako na kukutafuta. 

Pili utahitaji uwe na ukurasa kwenye Instagram wenye jina la biashara yako. Hapa utakua unaweka picha za bidhaa au huduma uanzotoa au wewe mwenyewe. Hii inawavuta watembeleaji waone kitu halisi unachokifanya.

Kwa wale ambao wanatumia groups za whatsapp kuweka maelezo ya bidhaa zao au kuweka mafundisho si vibaya ila inaweza kua ni upotevu wa kazi zako kama hujazitunza sehemu nyingine. Ukimiliki blog mtu yeyote anaweza kutembelea hata kama hayuko kwenye mtandao wowote pale tu unapompatia link ya ukurasa wako.


 Katika kipindi hiki cha karibuni kumekua na watumiaji wengi sana wa mtandao wa internet hasa baada ya kuja kwa wingi kwa simu za mkononi aina ya smartphone kwa maisha ya sasa karibia kila mahali unapokwenda huwezi kumkosa mtu na simu yenye uwezo wa internet.


Usiogope kuchukua hatua hata kama hujui chochote tutakufundisha ili uweze kufaidika na mabadiliko haya. Huko tuendako tutafika mahali lazima ujue kutumia mtandao maana huduma nyingi zitakua zinatolewa kwa njia ya mtandao. Sasa hivi tuaendesha semina kwa njia za mtandao. Kwenye groups za Whatsapp na Telegram. Dunia inafika sehemu ambapo lazima kila mmoja abadilike kuyafuata mabadiliko la sivyo utaachwa nyuma sana.



Faida za kumiliki blog:

     Biashara/Kipaji chako kutambulika kimataifa

Blog inawezesha biashara/huduma au kipaji chako kutambulika kimataifa kwa kua mtu yeyote popote duniani anaweza kutembelea blog yako na akaona kazi/huduma zako au bidhaa unazotoa au kile unachokiandika, hii itaifanya biashara yako kipaji chako au maandishi yako yatambulike zaidi na watu wengi hata usiowajua.


Utunzaji wa kumbukumbu
Chochote utakachokiweka kwenye blog yako kitakua salama hivyo basi kumbukumbu zako zinakua salama. Unaweza kuandika kwenye blog na kujitengenezea watembeleaji na kufungua fursa mbalimbali hapa Tanzania na nje ya nchi. Kumbukumbu zako utakua nazo wewe na utaweza kuacha alama duniani hata siku ukiondoka.



 Kuacha alama.

Unapomiliki blog unaacha alama duniani blog yako itaendelea kua hai na yale uliyoayaandika yatakuwepo. Nimeona shuhuda mbalimbali za watu waliosoma Makala kwenye mitandao wakachukua hatua zikabadili maisha yao, hivyo hata wewe unaweza kuacha alama, sio biashara pekee yake unaweza kumiliki blog kwa ajili ya kitu chochote unachotaka jamii ifahamu ni wewe unakifanya.




    Inakujengea nidhamu


Unapokua na blog yako unaandika kuhusu kitu Fulani ni muhimu ujiwekee ratiba maaalumu ya kuandika kama ni kila siku au kwa wiki mara moja  vyovyote vile itakujengea wewe nidhamu binafsi ya kufanya mambo mengine pia. Unaweza kuanzisha pia groups za Whatsapp ambazo ni kwa ajili ya watu wanaosoma vitu unavyoviandika.




KUTENGENEZA PESA


Ukimiliki blog unaweza kutengeneza pesa sana kama tulivyoona faida nyingine, unatengeneza pesa kwa huduma utakazo kua unazitoa, unaweza kutengeneza vitabu vilivyopo kwenye mfumo wa pdf ambapo wasomaji wako utawauziwa kwa njia ya email, unaweza kuendesha semina za online wasomaji wako wakalipia, unaweza kuuza bidhaa zako sehemu mbalimbali kwa watembeleaji wako, cha muhimu ni uvumilivu kwa kua haya hayatokei ndani ya siku moja bali yanaletwa na uaminifu uliojengeka kati yako wewe na watembeleaji wako.




  Data Tz Group inakuwezesha wewe na watu wako unaotaka waone kile unachokifanya kwa kukupa huduma nzuri ya kutengenezewa blog na utakayoweza kuendesha mwenyewe. Unachotakiwa kufahamu ni kutumia simu yako ya kiganjani (smartphone) au computer yako.



www.datatz1.blogspot.com  Gharama yake ni Tsh 50,000 ambapo hutalipia tena baada ya hapo kama unataka ibaki hivyo hivyo.


 www.datatz1.com Gharama yake ni tsh 100,000/= na utakua unalipia Tsh 30,000/= kila mwaka baada ya mwaka wa kwanza. Tofauti yake ni kwamba unakua umenunua Domain ya jina unalolitaka na ile blogspot inaondoka, hivyo unachokilipia kila mwaka ni hilo jina.

Vitu Utakavyopata tofauti na Blog ni



(a)  Ukurasa wa Facebook wa Biashara yako au Jina lako.

     

(b)  Mail List hii ni sehemu watu unaofanya nao biashara wanapojiunga hivyo unakuwa na uwezo wa kuwasiliana nao.

(c)  Mbinu mbalimbali za kukusanya watembeleaji kwenye blog yako.

(d)  Muonekano Bora wa Blog Yako pamoja na maelekezo juu ya kutumia. 
(e)  Utapata Email kama umenunua domain name na itakua ni fowarding email au yenye mailbox ya kujitegemea chaguo ni lako.





Mawasiliano yetu


Simu: 0763491136 (WhatsApp)


       Email: boniface.yohana@yahoo.com




Unatengenezewa blog popote ulipo duniani unatuma pesa kwa njia ya simu  M Pesa O763491136 Tigo pesa 0714067875 majina ni Boniface Yohana  kisha unatuma ujumbe mfupi wenye majina yako pamoja na maelezo kuwa umenitumia pesa.


Kwa walio nje ya nchi unaweza kuwasiliana nami kwa njia ya email boniface.yohana@yahoo.com au kwa Whatsapp +255 763491136


Asante sana na Karibu.

HIZI HAPA NI BAATHI YA BLOG NILIZOWATENGENEZEA WATU BINFSI NA VIKUNDI     MBALI MBALI. 

1. Data Tz GROUP

2. KILIMO TIJA

3. ECONOMIC NEWS

4. TORL GARDEN PLANNERS

5 CCM BOKORANI


3 comments:

© 2015-2016 DATA TZ GROUP. WP Theme-junkie converted by Bloggertheme9
Blogger templates. Proudly Powered by Blogger.
back to top